Skip to main content
     

Steve Mweusi

Steve Moses Musa (anafahamika zaidi kwa jina lake la kisanii kama Steve Mweusi; amezaliwa Majengo, wilaya ya Mpanda, Mkoa wa Katavi, 16 Septemba 1990) ni muigizaji wa vichekesho vifupi ambavyo hutazamwa zaidi katika mtandao ya kijamii [1]. Sanaa yake ambayo alikuja kuianza rasmi jijini Dar es Salaam mnamo mwaka 2018 iliweza kufungua ndoto zake za kuwa mmoja wa wasanii maarufu wa uigizaji wa vichekesho nchini Tanzania.